0




BIASHARA YA MTANDAO

Watu wengi sana leo wanaishi maisha yasiyo kuwa na ndoto kabisa. Hii ni kutokana na maisha yalivyo na mfumo wa uchumi umewafanya wasione kabisa uwezekano wa kuzifikia ndoto zao.
Sio kwamba hawajawahi kuwa na ndoto, hasha. Ila ndoto zao zimeuawa na mfumo au niseme ugumu wa maisha. Wengine hata hawazikumbuki tena ndoto walizowahi kuwa nazo.

Hebu jiulize,  kama fedha isingekuwa kikwazo je:-
Ø  Hiyo  nyumba unayoishi ndiyo ambayo ungeishi?
Ø  Ungevaa   kama unavyo vaa leo?
Ø  Ungefanya nini kwa wazazi au ndugu zako wasio na uwezo?
Ø  Ungejitoa kiasi gani kwa ajili ya Mungu?
Ø  Ungetaka kufika wapi na wapi duniani?

Utagundua wengi tunaisha maisha ambayo siyo ndoto zetu ila tumeamua kuyakubali kwa sababu hatuoni namna nyingine.

Wengi tuliweka tuliamini kuwa pengine kukipata kazi mambo yatakuwa sawa, lakini baada ya kupata kazi mwaka wa kumi sasa mambo bado ni magumu.

Leo nataka nikuoneshe fursa ambayo wengi hawajaiona. Na hii ni fursa ya kujiajiri bila kuathiri ajira yako ya sasa.

Fursa hii ni  kufanya biashara kwa muda mfupi sana kwa siku na katika masaa ya ziada.
Fursa hii kama ikitumiwa vizuri na kwa juhudi inaweza kufufua upya ndo zako.
Hapa nazungumzia kufanya biashara ya mtandao yaani NETWORK MARKETING.

Najua wengi wamewahi kusikia kuhusu biashara ya mtandao ila naomba uchukue nafasi hii tena kuifahamu zaidi.

Hata kama hutaki kufanya biashara hii nakushauri usome tu na kuilewa, pengine siku moja unaweza kuamua kufanya au hata kumsaidia mtu mwingine



BIASHARA NA MTANDAO NI NINI?
Biashara ya mtandao au network marketing ni mfumo mpya wa usambazaji  na ugavi wa bidhaa  unaoshamiri kwa kasi kwenye karne hii ya 21.  

Mfumo huu ulianza mwaka 1950 huko Marekani.  Kuna makampuni mengi sana duniani kwa sasa  ambayo yamesajiliwa kufanya biashara kwa njia hii ya mtandao.  

Mfumo huu unamruhusu mteja mwenyewe kuwa ndio msambazaji na muuzaji wa bidhaa.
Kwa mfumo huu, unakuwa umepunguza wauzaji waliopo kati ya kiwanda na mtumiaji, kama vile, wakala mkuu, wauzaji wa jumla, wenye maduka kisha mtumiaji.


kwa kifupi kwenye biashara ya mtandao, mteja ndiye anayekuwa msambazaji na mtangazaji wa bidhaa na kampuni inamlipa kamisheni kwa kadri ya manunuzi  wateja aliyowatambulisha bidhaa.

kama ambavyo unaweza kumwelekeza rafiki yako kwenye saluni nzuri, au mgahawa mzuri au hata duka zuri, unaweza pia kumwelekeza rafiki yako au ndugu yako kwenye bidhaa nzuri.

tofauti na saluni au mgahawa au duka ambao hawatakupa chochote hata kama mteja ulimwelekeza atanunua vitu vya milioni moja, kwenye biashara ya mtandao kila kitu atakachonunua mteja uliyemweleza wewe, utapata kamisheni ya asilimia fulani.



FAIDA ZA BIASHARA YA MTANDAO
Ø  Utaifanya kwa muda wa ziada bila kuathiri kazi au biashaza yako nyingine.
Ø  Unaweza kuanza na mtaji mdogo sana
Ø  Huta kuwa umeajiriwa
Ø  Huta  hitaji wafanya kazi.
Ø  Hulazimiki kukaa na bidhaa nyumbani kwako au kwenye duka.
Ø  Utajifunza elimu ya ujasiriamali kuliko ukiwa mahali pengine popote.
Ø  Utapata bonas/gawio kila mwezi kulinga na manunuzi yako pamoja na manunuzi ya watu ulio waelekeza
Ø  Inakupa uhuru wa kweli wa muda. Unaweza kuwa huru bila kazi lakini ukawa unaingiza fedha.
Ø  Utaingiza fedha kulingana na juhudi zako na sio kulingana na muda.
Ø  Haina kulipa kodi kwani kodi hulipwa na kampuni husika.



© Grant
+255 763 449 749
Facebook: Grant Sumaye
Instagram: grant_s.s

Change first. Change fast.

Post a Comment

 
Top